HISA NI UFUNGUO MAMA WA UCHUMI WAKO

Bado tuko wote kwenye Programu yetu ya TANZANIA TUWEKEZE. HAIPPA PLC tupo kujenga Uchumi usioyumba sio tu mtu kwa mtu mmoja mmoja bali kwa familia na Taifa kwa ujumla.  Mara nyingi utasikia serikali mbalimbali duniani zikiweka mikakati na jitihada za kuvutia Wawekezaji. Hii inakupa picha jinsi Uwekezaji ulivyo jambo la muhimu duniani. Nakukumbusha kwamba PROGRAMU hii ya kibingwa ya TANZANIA TUWEKEZE inaletwa kwako na HAIPPA PLC.

Kwa wanafunzi wetu wapya, HAIPPA PLC ni Kampuni ya Umma inayofanya shughuli za kubuni Miradi ya Uwekezaji jumuishi sambamba na Kuelimisha na Kushauri Umma kuhusu mambo ya Hisa na Uwekezaji. Leo tujadili pamoja kwanini HISA ni UFUNGUO MAMA WA NDOTO ZAKO KIUCHUMI.

Tuanze kwa Kujikumbusha HAIPPA Tunaposema Hisa Tunamaanisha nini?

Kwa lugha rahisi kabisa HISA ni dhamana ya kifedha (financial instrument) inayokupa haki ya kuwa na umiliki kwenye kampuni. Unaponunua Hisa unanunua sehemu ya Kampuni na unakuwa mmoja wa watu wanaomiliki hiyo Kampuni na biashara zake.

Tutazame sasa kwanini HAIPPA tunaamini Hisa ni Ufunguo Mama katika Uchumi wa Mtu mmoja mmoja, Familia naTaifa. Tuanze na Faida kwa Mwekezaji mmoja mmoja:

  1. Hisa inampa fursa Mwekezaji kumiliki biashara ambayo tayari inatembea na kumwondolea usumbufu na gharama kubwa za pesa, muda na usimamizi katika kuanzisha biashara mpya.
  2. Hisa inampa Mwekezaji fursa ya kuwatumia watalaam bila malipo. Uanzishwaji na Uendeshaji wa biashara unahitaji wataalam wa fani mbalimbali kuwezesha masoko, utawala wa fedha, uzalishaji, usimamizi, uhasibu, taratibu za kisheria, mifumo ya kiteknolojia n.k. Mwekezaji anaponunua Hisa za Kampuni tayari anakuwa amewaajiri Watalaamu hawa wote ambao hutumika kuukuza mtaji wake.
  3. Hisa inampa mwekezaji fursa ya kutawanya hatari za Uwekezaji wake. Kupitia Hisa Mwekezaji mwenye mtaji wa shilingi milioni moja au milioni 50 kwa mfano anapata fursa ya kuutawanya mtaji wake kwa kununua Hisa kwenye biashara au kampuni zaidi ya moja na hii huongeza usalama wa mtaji wake.
  4. Hisa inampa Mwekezaji faida ya MUDA na NAFASI kuendelea kufanya majukumu mengine kwa ufanisi. Sio rahisi mtu mmoja kusimamia biashara 10 au kufanya ajira 10 kwa wakati mmoja lakini ni rahisi sana kwa Mtu kuwekeza kwenye Kampuni 10 za Hisa. Mfano Mtumishi anapoamua kuanzisha biashara itamlazimu kutenga muda wa kutosha kusimamia ufanisi wa hiyo biashara. Hii inaweza kuathiri utendaji wake kwenye majukumu ya utumishi. Lakini Mwekezaji anapoamua kununua Hisa jukumu lote la usimamizi ni jukumu la menejiment ya Kampuni ya Hisa.
  5. Hisa zinalinda Mtaji biashara zikipata hasara. Pana tofauti kubwa sana kwa watu wawili inapotokea hasara kwenye biashara zao. Kwa mfano Mtu mmoja mtaji wake shilingi milioni 10 ameweka kwenye biashara ya kilimo moja kwa moja. Na mwingine mtaji wake shilingi milioni 10 amewekeza kwenye Kampuni ya Hisa ambayo inafanya biashara ya kilimo. Ikitokea hasara kwenye biashara hizi hawa watu wawili wanapata hasara kwa kiwango tofauti. Anayefanya biashara ya kilimo moja kwa moja hasara yote kwa asilimia 100 inamhusu wakati mwekezaji wa Hisa hata kama Kampuni yake imepata hasara yeye anakuwa hajapata hasara mpaka atakapouza hisa zake kwa bei pungufu ya mtaji aliowekeza. Kwa msingi huu Hisa husaidia kulinda mitaji isipotee biashara zinapopata hasara.
  6. Hisa inakuza mitaji midogo iliyowekezwa kuwa mitaji mikubwa. Hii hutokea kupitia bei za Hisa kupanda, Hisa za bonasi, gawio kwa njia ya Hisa, bei za upendeleo kwa Wanahisa (right issue). Hizi faida zote kwa pamoja husaidia kukuza mitaji midogo kuwa mitaji mikubwa.
  7. Hisa zinatunza thamani ya Fedha dhidi ya mfumuko wa bei. Bei ya Hisa mara nyingi huakisi mwitikio wa hali halisi kiuchumi inayotokana na nguvu ya soko, ukuaji wa  kampuni, ukuaji wa sekta na mwenendo wa uchumi kwa ujumla. Huu mwitiko huifanya hisa kutunza thamani halisi ya mtaji wa Mwekezaji kupitia kupanda na kushuka kwa bei.
  8. Hisa huwapa Fursa Makundi yote na Wanafamilia wote kumiliki mali. Ni rahisi sana kwa Mwanafunzi wa Sekondari au Chuo kumiliki Hisa huku akiendelea na masomo yake. Ni rahisi sana Mtu mwenye ulemavu kuwekeza kuliko kufanya biashara au ajira. Ni rahisi sana kwa Mwanamke kumiliki hisa na pia ni rahisi sana hata kwa mtoto kuwekeza. Kwa msingi huu kila mtu katika familia au jamii bila kujali hali yake, jinsi, umri au ujuzi anaweza kumiliki hisa ambayo ni mali na kitega uchumi cha kudumu.
  9. Hisa zinajenga Utajiri. Wote tunafahamu kwamba Matajiri wengi duniani wamejenga utajiri wao kupitia Hisa za Makampuni yao.
  10. Faida kwa nchi; Kampuni za Hisa na masoko ya hisa vimekuza ubunifu, vimejenga biashara kubwa  na kutawanya faida za Kiuchumi kwa Wananchi wengi.

Faida zote hizi zinabainisha msimamo wa HAIPPA PLC kwamba Hisa ni Ufunguo wa Mama katika Uchumi wa Mtu, Familia na Taifa. Sasa tupigie mstari baadhi ya Mambo ambayo ni muhimu kufahamika kwa Mwekezaji anayeanza kujifunza kuhusu Uwekezaji.

Ni Kampuni Gani zinaruhusiwa Kuuza Hisa zake kwa Umma?

Kampuni zinazoruhusiwa kuuza hisa zake kwa Umma ni zile ambazo katika Usajili wake zimepewa hadhi ya kuwa Kampuni za Umma yaani Public Limited Company au kwa kifupi PLC.

 

Tunapata wapi Taarifa kuhusu Kampuni za Kuwekeza?

Taarifa kuhusu Kampuni za kuwekeza hupatikana kupitia Masoko ya Hisa na Kampuni changa au mpya taarifa zake hupatikana kupitia website za Kampuni husika,  vyombo mbalimbali vya Habari au madalali wa Hisa.

 

Masoko ya Hisa ni Kitu Gani?

Masoko ya Hisa ni majukwaa ambapo Hisa za Makampuni mbalimbali huuzwa na kununuliwa.

 

Je Kampuni zote za Hisa zipo kwenye Masoko ya Hisa?

Hapana sio Kampuni zote za Hisa zipo kwenye Masoko ya Hisa. Kampuni changa au mpya nyingi hazipo kwenye Masoko ya Hisa.

 

Sheria zinasema nini Kuhusu Kampuni za Umma kuwepo kwenye Masoko ya Hisa?

Sheria hailazimishi Kampuni ya Umma kuwepo kwenye Soko la Hisa kwasababu Kuorodhesha hisa za Kampuni kwenye Soko la Hisa sio lazima ni hiari kabisa na Lini zitaorodheshwa yanabaki kuwa Maamuzi ya Bodi na Wanahisa wa Kampuni husika.

Je ni Salama kuwekeza kwenye Kampuni za Umma ambazo hazipo kwenye Masoko ya Hisa?

Jibu ni ndiyo. Ni salama kuwekeza kwenye Kampuni ya Umma hata kama Hisa zake hazipo kwenye Soko la Hisa. Mambo ya kuzingatia ni Kampuni husika iwe imesajiliwa kama ni Kampuni ya Umma na maono na biashara za Kampuni husika zinalandana na malengo yako kwamba ni ya muda mfupi au muda mrefu. Kwenye kuchagua Kampuni ya Kuwekeza Wawekezaji hugawanyika katika makundi mawili; Wawekezaji wanaopenda Hisa za Makampuni makongwe yaliyo na muda mrefu sokoni hata kama zinalipa faida ndogo. Kundi la pili ni Wawekezaji wanaopenda Kampuni zinazokua haraka na kulipa faida nzuri hata kama ni changa au mpya sokoni. Kundi hili la pili hupendelea kununua hisa za Kampuni kabla au wakati wa kutambulishwa kwenye masoko ya Hisa.

 

Kwanini Watanzania wengi Hawajachangamkia Uwekezaji kwa njia ya Hisa?

Kwa utafiti uliofanywa na HAIPPA PLC unaonyesha ziko sababu kadhaa zilizosababisha Watanzania wengi kushindwa kuwa kwenye Uwanja wa Uwekezaji kwa njia ya hisa.

a) Watanzania wengi hawajafundishwa na hawaelewi kabisa kitu Hisa wala Uwekezaji na wengi wamekuwa katika imani kwamba 'Mwekezaji ni Mtu tajiri'. Ukweli ni kwamba hata ukiwa na Tsh20,000 unaweza kuanza safari yako ya kuwa Mwekezaji.

b) Tanzania bado tuna uchache wa Makampuni ya Hisa.

c) Wawekezaji  wadogo waliowahi kuthubutu kuwekeza kabla kukaa muda mrefu bila kupata Gawio wala taarifa kutoka kwa Kampuni zao kuhusu maendeleo ya Uwekezaji wao.

d) Wengi kwa kutokujua jinsi ya kupima faida za Uwekezaji hutumia gawio kama kipimo cha kuchagua kampuni na huacha faida na vipimo vingine kama vile ongezeko la mtaji kupitia bei ya Hisa.

 

HAIPPA PLC Tunafanya nini Kuchangamsha Uwekezaji nchini?

HAIPPA PLC tumeanzisha Akademi ya Uwekezaji na Programu ya Tanzania Tuwekeze ili kutoa mafunzo ya Uwekezaji kwa Vitendo. Kupitia Program hii kila Mtanzania anapata fursa ya kufungua Akaunti ya HAIPPA bila gharama na kununua Hisa za awali kati ya 50 na 1000. Ili kuongeza mvuto tumefanya ubunifu, Gawio la HAIPPA linalipwa kila mwezi kiwango cha 3% na linalipwa kwa njia ya Hisa mpya ambazo unaweza kuziuza na kujipatia fedha taslimu . Kuhusu taarifa kwa Wawekezaji HAIPPA PLC tunatoa taarifa za kutosha kupitia mifumo ya kidigitali na vituo vyetu vya Huduma kwa wateja. Ili kukabiliana na Tatizo la uchache wa Makampuni ya Uwekezaji, HAIPPA tunasaidia kubuni Makampuni mapya na Miradi mipya ya Uwekezaji jumuishi kwenye Sekta mbalimbali ili kupanua wigo kwenye Uwanja wa Uwekezaji.

Nini Wito wa HAIPPA PLC kwa Umma?

HAIPPA PLC tunawaalika Watanzania kufungua akaunti za HAIPPA ili kujipatia elimu, taarifa na fursa mbalimbali zinazojili kwenye dunia ya Uwekezaji. Kauli mbiu yetu HAIPPA tnasema Kila Mtanzania Sasa ni Mwekezaji.

Mawasiliano

Tunakukumbusha Umma kwamba Akaunti ya HAIPPA na Elimu ya awali vinatolewa bure. Huduma zetu zinapatikana Mikoa yote kupitia simu yako iwe kubwa au ndogo. Kupata Elimu zaidi, Kufungua Akaunti na Huduma zetu

Tutembelee www.Haippa.net

Jaza fomu ya Kujiunga https://in.haippa.co.tz/authentication/signup

Au Piga *149*46*23# au Simu 0755947943; App yetu Play store ni HAIPPA PLC

Ofisi zetu zipo DSM (Kisutu), Mwanza (Nyamanoro) na Mara (Mwembeni Complex Musoma Mjini). Pia tuna Mawakala Mikoani

KARIBUNI HAIPPA

Akademi ya Uwekezani Tanzania, Fursa za Uwekezaji kwa Wote

WEKEZA KWA KUJIAMINI

HUDUMIWA KIDIGITALI UKIWA POPOTE!